vid

Ishu ya msanii Young Siza kumdai producer wake imesikika kwenye U Heard…


SoundRecording-MicTaarifa zilizomfikia Soudy Brown kuwa msanii  Young Siza amezulumiwa na producer Mesen Selector kiasi cha shilingi laki tano na kumi alizompa kwa nyakati mbili tofauti.
Young Siza amesema alikuwa anafanya kazi na Mesen, wakati anataka kutoa video yake ya ‘Kanya Boya’ akamuazima shilingi laki tatu, kwa makubaliano ya kumrudishia.. wakati anataka kurekodi wimbo mpya akamwambia ameshakuwa msanii wake na kumtaka alipie shilingi laki mbili na kumi badala ya laki tatu akalipa na kurekodi wimbo lakini baadae akaambiwa wimbo huo umefutwa.
Akaanza kumfatilia ili ampe fedha zake bila mafanikio na kuamua kwenda kituo cha Polisi Mabatini kutoa taarifa, baadae alifanikiwa kumkamata wakaongea akamlipa shilingi laki tatu bado anamdai laki mbili na kumi na akimpigia simu hapokei wala kujibu message.
Kusikiliza story yote ya U Heard bonyeza play hapa chini

__________________________________________________________________________________________________________________________________

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni