Mchekeshaji Kingwendu amesema wasanii waotaka kumshirikisha kwenye video au movie, kitu cha kwanza kuangalia ni ujumbe na kama msanii huyo anajulikana endapo hajulikani gharama zake zinaanzia milioni moja hadi laki tano ila kwa msanii mkubwa huwa anafanya laki mbili au tatu kwasababu anajua kuna siku na yeye atamhitaji kwenye kazi zake..
Producer One ambae amehusika kufanya mixing ya wimbo mpya wa Chid Benz amesema, ameanza kufanya production muda mrefu lakini hakutaka kufanya rasmi kutokana kushindwa kufanya majukumu mengine, lakini kwasasa atakuwa anafanya production kama alivyofanya kwenye Album za wasanii mbalimbali.
Msanii wa mziki wa dance nchini Christian Bella amesema video ya wimbo wake mpya wa ‘Nashindwa’ ndio video aliyofanya kwa gharama kubwa toka aanze mziki, video ambayo imefanywa na director mkali Bongo Adam Juma ambayo ameifanyia nchini Afrika Kusini.Kusilikiza story zote za 255 bonyeza play hapa chini...
____________________________________________________________________________________________
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni