vid

neyBaada ya msanii Nay Wa Mitego kuwa kwenye maelewano mabaya na mzazi mwenzie na kuamua kumchukua mtoto wake  lakini mama yake alikuja kudai kuwa sio mtoto wake Nay na kuamua kwenda kufanya vipimo vya DNA ili kujua kama sio baba halali wa mtoto huyo.. baadae taarifa zikasambaa kuwa yuko kwenye mahusiano na muigizaji Shamsa Ford.
Diamond ni mtu wa kwanza kuvujisha picha ya kimapenzi ya nay na Shamsa katika ukurasa wake wa Instagarm alipoulizwa akajibu hivi… ‘ila Nay anyway tulikaa sisi na Nay tunazungumza nini kwenye simu yake na Nay naona sijui nilikua naangalia nini  katika simu yake alinigea naangalia hii katika kupita zangu nakutana na ile picha nikajitumia nikaipost ndio hivyo tuu basi”
Akizungumza na Soudy Brown kuhusu ishu hiyo Nay amesema watu wanaongea lakini hakuna ukweli wowote hata Diamond anajua hawako kwenye mahusiano ila tu nimkorofi.
Akizungumzia kipimo cha DNA alichoenda kufanya na mtoto wake amesema aliamua kufanya hivyo kwa usalama wa mtoto kutokana na kile kilichotokea ili asije kupata shida badae kipimo ambacho kilichukua zaidi ya wiki mbili na wakili wake ndi alienda kuchukua majibu.. amesema alikuwa na wasiwasi kwasababu siku zote mama ndio anaemjua baba wa mtoto, lakini anamshukuru Mungu yuko wa watoto wake na yeye ni baba mzuri na hana tatizo na mwanamke yeyote ..ameanza maisha mapya na watoto wake.
Kusikiliza stori yote bonyeza play hapa chini…
 
__________________________________________________________________________________________

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni